Je, unafurahia vile mwili wako una nguvu, Je, unapenda kusikiliza upepo wa Pwani? Na kufurahia sauti ya mvua juu ya paa yako, je na sauti ya upepo mwana au pia kufurahia mziki ya kupendeza.


In नJehanum hakutakuwa na mambo kama haya. Bibilia inatuambia kitakachosikika ni kilio na kusaga meno kwa watu.



Bwana wake mtumwa huyo atakuja siku usiyodhani, na saa asiyoijua.51. Atamkata vipande viwili, nakumwekea fungu lake pamoja na wanafiki; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.-Mathayo 24:50,51


Biblia inatuambia Bwana atakuja kwa wakati na siku ambaye hatuwezi tukatarajia, Hakuna njia ya mkato ya kurudi kwa Bwana Yesu. Siku ya kuja kwa Yesu mara ya pili ni karibu sana, kama haujaokoka usisubiri mda mrefu. Kile unaweza kufanya sasa, fanya sasa. Maandiko yanatuambia siku ya wokovu ni sasa.


"Kwa maana asema, wakati uliokubalika nalikusikia, siku ya wokovu nalikusaidia; Tazama, wakati uliokubalika ndio sasa; tazama, siku ya wokovu ndiyo sasa. – 2 Wakorintho 6:2

Amua sasa wakati ni wako Yesu anangojea majibu yako sasa.


Ijayo